Samsung inathibitisha kuwa wadukuzi walihatarisha mifumo yake na kuiba source code za Galaxy
Samsung ilithibitisha Jumatatu kwamba baadhi ya data zake ziliibiwa kama sehemu ya shambulio la mtandao ambalo liliripotiwa kwa mara ya kwanza mwishoni mwa wiki. Katika taarifa kwa Bloomberg, kampuni kubwa ya vifaa vya elektroniki ya Korea ilifichua kwamba ukiukaji wa usalama ulisababisha “baadhi ya source code (msimbo) zinazohusiana na uendeshaji wa vifaa vya Galaxy”.