Usitumie Windows 7 wala TeamViewer, ujumbe kutoka FBI. #Usalama #Udukuzi
Ushawahi tafuta sababu kwa nini usitumie Windows 7 kwenye kompyuta yako? Basi FBI wanakupa sababu.
Ushawahi tafuta sababu kwa nini usitumie Windows 7 kwenye kompyuta yako? Basi FBI wanakupa sababu.
Mdukuzi mmoja Marekani adukua mfumo wa maji wa jiji la Oldsmar kwenye jimbo la Florida na kutaka kuongeza kiwango cha kemikali kwenye maji hayo ili kuyafanya kuwa hatari kwa afya ya binadamu.
Watumiaji kadhaa wa simu zinazotumia Android wameripoti kuhusu picha inayoharibu simu. Yaani picha hii inaweza ‘kuzingua’ ufanyaji kazi wa simu yako.
Simu za Xiaomi zinarekodi data za mamilioni ya watumiaji wake, hicho ndicho kilichosemwa na ripoti mpya kutoka kwa mtafiti wa mambo ya kiusalama.
Shirika la ujasusi na uchunguzi wa ndani la Marekani la FBI, limewataka watu kuwa makini na Smart TV majumbani kwao. Wadai wadukuzi wanaweza kudukua TV janja kwa urahisi.
Teknolojia ya Fingerprint yashindwa kufanya kazi kwa usahihi kwenye baadhi ya simu maarufu za Samsung. Apps za huduma za kibenki zaanza kuzuiwa kufanya kazi.
Data za akaunti milioni 210 za watumiaji wa mtandao wa Facebook zavuja baada ya kudukiliwa na taarifa za akaunti zao zinapatikana kwa urahisi mtandaoni.
Korea Kaskazini wakana kuiba kwa kutumia udukuzi. Serikali ya Korea Kaskazini imekana shutuma ya kuhusika na wizi wa zaidi ya dola bilioni 2 za Kimarekani kwa njia ya mtandao.
Google wamesema wamefanya uamuzi wa kuchelewa kuruhusu apps mpya kuanza kupatikana kwenye Google Play Store kwa sababu za kiusalama.
Gazeti mashuhuri la nchini Marekani, Wall Street Journal katika uchunguzi wao wamebaini wafanyakazi wa Huawei wanahusika na udukuzi na kusaidia shughuli za kijasusi dhidi ya wanasiasa barani Afrika.
Je ushawahi kufahamu kuna tovuti inayokusaidia kuokoa mafaili yaliyodukuliwa inayokwenda kwa jina la No More Ransom? Tovuti hii ina programu mbalimbali za kusaidia kuokoa mafailia yaliyodukuliwa na kubadilishwa na kutoweza kutumika.
Je umeshatumia app ya FaceApp.? Hadi sasa utakuwa umekutana na picha za wazee kwa wingi kwenye mitandao ya kijamii. Lakini tofauti ni kwamba hizi ni picha za watu ambao si wazee kwa sasa.
Ushawahi kusikia kuhusu kampuni ya Cellebrite kutoka nchini Israeli? Tusharepoti kuhusu kampuni hii na biashara waliyofanya na FBI, na sasa wamekuja na taarifa mpya. Wanamiliki teknolojia yenye uwezo wa kudukua simu yeyote inayotumia toleo la iOS 12.
Fahamu Intel waitetea Huawei dhidi ya katazo la kibiashara la serikali ya Marekani. Nje ya Google ni makampuni mengi sana mengine ambayo yameathirika na katazo la kujihusisha na Huawei kibiashara.
Je utafahamu vipi kama password yako imedukuliwa? Inaweza ikawa ni kwenye tovuti ya mtandao wa kijamii au tovuti nyingine ya aina yeyote, kila mwaka udukuzi unaohusisha maelfu ya akaunti za mitandaoni hufanyika.
Udukuzi WhatsApp. Jumanne hii WhatsApp ambayo ipo chini ya Facebook imeomba usaidizi rasmi wa wizara ya Sheria ya Marekani katika uchunguzi juu ya udukuzi uliofanywa na watu wanaonekana kuwezeshwa na serikali.
Binance, moja ya kampuni kubwa inayojihusisha na kusimamia akiba na mihamala ya pesa ya kidigitali ya Bitcoin imedukuliwa na mabilioni ya pesa – dola milioni 41 za Marekani – takribani zaidi ya bilioni 80 za kitanzania.
TCRA kupitia kitengo chao cha ulinzi wa kompyuta wa dharura, TZ-CERT imeleta shindano kwa wanavyuo wachukuao masomo ya teknolojia ambalo litawafanya wanafunzi kuweza kudukua taarifa na kujilinda na mashumbulizi kupitia shindano la kudukua (HACKING COMPETITION).
Kama wewe ni mtumiaji wa WhatsApp basi tayari utakuwa umeona ujumbe unaosambaa ukidai kama umepoteza simu yako basi tuna namba ya IMEI kwenda cop@vsl.net. Je kuna ukweli wowote?