Samsung ilithibitisha Jumatatu kwamba baadhi ya data zake ziliibiwa kama sehemu ya shambulio la mtandao ambalo liliripotiwa kwa mara ya kwanza mwishoni mwa wiki. Katika taarifa kwa Bloomberg, kampuni kubwa ya vifaa vya elektroniki ya Korea ilifichua kwamba ukiukaji wa usalama ulisababisha “baadhi ya source code (msimbo) zinazohusiana na uendeshaji wa vifaa vya Galaxy”.
Ingawa Samsung haijafichua wahusika waliosababisha shambulio hilo, kundi la wadukuzi la Amerika Kusini Lapsus$ limedai kuhusika. Shirika lilisambaza faili lenye ukubwa wa GB190 ambayo inaripotiwa kuwa inajumuisha msimbo wa vifaa vyote vya hivi karibuni vya Samsung, pamoja na msimbo unaohusiana na uthibitishaji wa kibayometriki. Huenda wavamizi pia wamepata ufikiaji wa data ya siri inayohusiana na Qualcomm.
Kukubali huko kumetokea ndani ya wiki moja baada ya kikundi hicho kusema kuwa kilipata data takriban TB1, pamoja na michoro na msimbo, kutoka kwenye kampuni kubwa ya NVIDIA. Kampuni hiyo ilisema ilifahamu shambulio hilo mnamo Februari 23, baada ya hapo Lapsus$ ilidai fidia iliyolipwa kwa njia ya cryptocurrency ili kuzuia faili za NVIDIA zisionekane hadharani. NVIDIA iliposhindwa kujibu, msimbo wa chanzo wa teknolojia ya DLSS ya kampuni na maelezo yanayohusiana na hadi kadi sita za michoro ambazo hazijatangazwa zilisambazwa mtandaoni.
“Kwa sasa, hatutarajii athari yoyote kwa biashara au wateja wetu. Tumetekeleza hatua za kuzuia matukio kama hayo zaidi na tutaendelea kuwahudumia wateja wetu bila usumbufu,” Samsung ilithibitisha baadaye katika taarifa yake. Haijulikani ikiwa Lapsus$ ilitoa madai yale yale ya cryptocurrency kwa Samsung, lakini tumewasiliana na kampuni hiyo ili kupata ufafanuzi.
Chanzo: Engadget
No Comment! Be the first one.