Netflix wapandisha bei kwa baadhi ya vifurushi Marekani.
Kampuni ya Netflix mwishoni mwa wiki iliyopita ilipandisha bei ya baadhi ya vifurushi vyake kwa watumiaji wa Marekani. Mabadiliko hayo ambayo wenyewe wanasema hayaji kwa uharaka katika mataifa mengine yanaonekana yamekuja katika kipindi ambacho tayari kuna ushindani mkubwa nchini humo kutoka huduma zingine kama vile Apple TV, Amazon Prime na nyingine nyingi.