Kwa sasa mtandao maarufu sana wa Netflix umepata pigo kubwa la kupungua kwa mapata na kushuka kwa wateja wake (subscribers).
Pengine hii ni njia moja wapo ya kuhakikisha kuwa wanaguza karata ili mambo yarudi kama yalivyokua mwanzo.
Kumbuka pia kampuni hiyo ina pinga vikali swala la akaunti moja kutumika na zaidi ya watu wawili au zaidi ambao ni tofauti.
Lakini sio Netflix peke yao ambao wanasema huduma hii itaanza rasmi katika miezi mitatu ya mwisho mwaka 2022., Wenzao Disney Plus walisema wanafikiria huduma hiyo mwezi wa tatu mwaka huu.
Kama ilivyo kawaida inasemekana kuwa makampuni mengi ambayo yanatoa huduma sana yatafuata nyayo hizi.
Kwa Netflix kitakachofanyika ni kwamba kampuni hii itashusha bei za vifurushi vyake lakini vifurushi hivyo vitakua vinaruhusu matangazo kuonekana.
Ukifikiria kwa undani ni jambo zuri maana hapa kila mtu anashinda kwa upande wake. SOMA KILA KITU KUHUSU NETFLIX >>HAPA<<
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako niandikie Hapo chini katika uwanja wa comment, hili umelipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
One Comment