Kazi mia tatu sio mchezo, hili limefanyika baada ya kampuni kupoteza ‘subscribers’ (wateja) 200,000 ikiwa ni namba kubwa ambayo haikutegemewa.
Kumbuka mwezi mei kuna mikataba mingi ilisitisha na kazi kama 150 hivi zilipunguzwa na kampuni hiyo ya Netflix
Tumeona kwa mwaka huu kampuni nyingi zinapitia kipindi kigumu kama vile kushuka kwa mauzo na kadhalika hali ambayo inapelekea vitu kama kupunguza nafasi za kazi.
Kushuka kwa uchumi bado ni moja kati ya sababu kubwa kabisa inayopelekea haya maana kila kampuni haipati kama ilivyokua inapata mwanzo wakati hali ilivyokuwa shwari
Netflix wanasema kuwa wanafanya hivi ili kuhakikisha kuwa ukuaji wao na uwekezaji wao inabidi uendane sambamba na mapato yao.
Ni wazi kuwa kwa mitandao mingi ya kiteknolojia imekua ikishuka mapato, hali ambayo imepelekea mitandao mingi kuwa na hudumu ya ziada ya kupata mapato
Mfano huduma nyingi za mitandao ya kijamii zimeanzisha vipengele vya kulipia, mfano mzuri ndani ya WhatsApp Business na Telegram Premium n.k.
Netflix pia wanasema licha ya wao kuwa wanapitia katika kipindi kigumu ila wanatamani kwamba waweze kurudi katika hali yao ya kawaida katika kazi zao.
Ningependa kusikia kutoka kwako niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili wewe unalipokeaje? Unadhani ni sahihi kwa makampuni makubwa hivi kuzidi punguza nafasi za ajira?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.