Netflix imekuwa ikipitia kipindi kigumu sana pengine tangu kuanziishwa kwake ni wakati huu ambao imekuwa ikiendelea kupoteza wateja wake. Na katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka huu Netflix imepoteza karibu wateja milioni 1.
Kwenye ulimwengu wa sasa si lazima tena kushusha filamu/tamthilia na kusubiri mpaka mchakato huo ukamilike ndio uweze kuingalia kupitia kifaa unachotumia. Netflix imekuwa mkombozi wa watu wengi duniani ambapo mtu anaweza kuangalia iwe ni filamu, tamthilia au sinema papo hapo bila ya hata kuishusha ingawa si BURE bali kwa malipo ya kila mwezi.
Sasa katika hilo la wateja, Netflix imejikuta ikipoteza wateja wake takribani 970,000 kati ya mwezi Aprili na Juni mwaka huu ambapo kwa lugha ya kiuchumi na kibiashara tunasema “Robo ya pili ya mwaka”. Kwa kipindi fulani janga la virusi ya Corona lilionekana kuwa neema kwa Netflix kutokana watu kutumia muda mwingi kuwa majumbani mwao hivyo kusababisha kuwa na wakati wa kutazama vipindi mbalimbali wanavyovifuatilia kwenye Netflix.
Kuongezeka kwa mapato ya Netflix kunatokana na ongezeko la wastani wa wateja ambao wanalipia kupata huduma halikadhalika wastani wa pato kwa mteja (Kiingereza: Average paid memberships and Average Revenue per Membership). Kwa upande mwingine mapato ya Netflix yangeweza kuwa juu zaidi lakini walijikuta wanapoteza $339 milioni kutokana na panda shuka ya fedha za kigeni.
Mipango ya kuongeza mapato
Netflix imejipanga kuendelea kutafuta mbinu ya kujiongezea mapato ambapo hivi karibuni iliingia makubaliano na Microsoft ambapo mapema mwaka 2023 matangazo ya bei rahisi yataanza kuonekana kwenye Netflix. Halikadhalika, katika kipindi hicho hicho Netflix inajipanga kukabiliana na wateja wanaolipia kupata huduma kisha kuwapa watu wengine nenosiri na barua pepe zao wanazotumia kwenye Netflix. BOFYA HAPA kufahamu zaidi.
Watu milioni 100 wanatumia huduma ya Netflix bure kutokana na kutumia kutumia akaunti milioni 200 waliolipia huduma.
Je, wewe ni kati ya watu ambao wanaangalia sinema, tamthilia, n.k kupitia Netflix? Unazungumziaje hiki ambacho Netflix inapitia hivi sasa? Tupe maoni yako.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
2 Comments