Mapato mengi kutoka katika kampuni ya Netflix yanapotea sababu wateja wake wengi huwa wanapeana neno siri (password) ili kufurahia huduma hiyo.
Yaani hapa ilikua anaweza kulipia mtu mmoja na kisha kuwa watu wengine neno siri ambalo litawawezesha kuingia katika akaunti hiyo kwa kutumia kifaa kingine na kisha kuweza kutumia huduma hiyo.
Hii ni moja ya njia mpya ambayo kampuni ya Netflix imeamua kuja nayo katika kuhakikisha kuwa inakusanya mapato yake stahiki.
Kwa sasa kampuni inafanya majaribio katika baadhi ya nchi na hapa kinachofanyika ni kwamba kampuni itaruhusu kabisa uwezo wa k’sign in’ katika kifaa kimoja (Tv) labda cha nyumbani na kisha…
…kuruhusu ku’sign in’ katika kifaa kingine tofauti na kile cha nyumbani, hili litafanikiwa lakini baada ya wiki mbili tuu…
…….Netflix itakutoa moja kwa moja na kukulazimu ulipie dola 2.99 za kimarekani ili kuendelea kufurahia huduma hiyo ukiachana na ile ambayo unalipia awali.
Kinachofanya hapa ni kwamba mtandao unauwezo wa kutambua kifaa kwa kutumia IP Address na utambuzi mwingine wa vifaa kutofautisha vifaa hivyo.
Kingine ni kwamba kampuni iko katika mchakato wa kukuza mapato yake maana yameshuka sana ukilinganisha na kipindi cha nyuma ndio maana kwa sasa wako na mpango hata wa kuja na Netflix yenye matangazo….soma Zaidi >>HAPA<< na >>HAPA<<
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili umelipokeaje? je utaweza kulipia zaidi kwa kifaa kingine ili uweze kufurahia huduma hii.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.