Netflix yazindua Kifurushi cha Bure nchini Kenya. Kampuni ya hii inayojihusisha na kuonyesha filamu pamoja na tamthilia mbalimbali mtandaoni imezindua kifurushi chao kipya cha bure kabisa kwa watumiaji wa simu janja za Android nchini Kenya tu kwa sasa.
Kampuni hiyo ya Netflix inategemea ya kwamba kwa kutoa kifurushi hicho cha bure chenye robo ya jumla ya filamu na tamthilia zinazoweza kupatikana nchini kenya itapelekea wakenya kuvutiwa na huduma zao na hivyo kujiunga na huduma zao za kulipia.
“Ikiwa haujawahi kutazama Netflix hapo awali – na watu wengi nchini Kenya hawajawahi – hii ni njia nzuri ya kupata huduma yetu,” Cathy Conk, mkurugenzi wa uvumbuzi wa bidhaa katika Netflix, aliandika katika chapisho la blogi. “Na ikiwa unapenda kile unachokiona, ni rahisi kuboresha hadi moja ya vifurushi vetu vya kulipia ili uweze kufurahiya huduma yetu kamili kwenye Runinga yako au kompyuta ndogo pia.”
-
Si muvi/filamu/tamthilia zote zinazopatikana kwenye akaunti zinazolipiwa zitapatikana kwenye akaunti hizi za bure.
-
Pia imekuwa kama ni njia ya kushindana na watu wanaofungua akaunti na kuzigeuza kama biashara kwa kuwachaji watu wengine ili kuwawezesha kutumia kwa muda wa saa/siku n.k. Baadhi ya watu nchini Kenya walianza kugeuza akaunti zao za Netflix kama biashara.
Katika kifurushi hicho kipya kilichozinduliwa na Netflix nchini kenya kutakuwa na upungufu flani wa masharti ya kufungua akaunti ya Netflix kama kutoweka taarifa zako za malipo. Lakini pia wameweka masharti ya utumiaji ambapo hautaweza kuangalizia filamu zao kwenye runinga lako pamoja na sehemu nyingine yeyote zaidi ya kwenye simu yako janja.
Soma mengine kuhusu Netflix kupitia Teknokona/Netflix
Hii inawaruhusu kuwapata watumiaji wengi wa mara ya kwanza ambao baada ya muda wanaweza kuvutiwa na kupata akaunti kamili ya Netflix. Je wataleta aina hii ya akaunti kwa mataifa mengine Afrika? Nadhani itabidi wajifunze kutoka Kenya kabla ya kufanya maamuzi kama hayo kwa mataifa mengine.
Chanzo: Netflix
No Comment! Be the first one.