Netflix imeweka vipengele kadha wa kadha na vile vile imetangaza kipengele amabacho kitakua na uwezo wa kuruhusu matangazo katika mtandao wake.
Lakini vyanzo mbali mbali vinasema kuwa matangazo hayo yataonekana kwa kila aina ya onesho. Kumbuka kuna baadhi ya maonesho ambayo yanamilikiwa na Netflix moja kwa moja na mengine yanamilikiwa na wengine.
Kingine ni kwamba katika mtandao huo kuna maonesho mahususi kwa ajili ya watoto tuu n.k. sasa kuna udadavuzi ambao upo juu ya matangazo yataonekana wapi na wapi.
Kutokana na ripoti ambazo zipo ni kwamba mtandao wa Netflix utaanza kuonesha matangazo katika maonesho yote isipokua yale ambayo ni mahususi kwa watoto na pia yale yale maonesho yanayomilikiwa na Netflix moja kwa moja.
Lakini vyanzo vingine vinasema kuwa maonesho ambayo yanamilikiwa moja kwa moja na mtandao huo hayatakua na matangazo lakini ni kwa kipindi cha mwanzo mwanzo wakati maonesho hayo yanaanza kutoka muda ukipita hata yenyewe yatakua yakipitisha matangazo.
Kwa sasa hakuna uhakika kwa asilimia mia juu ya hili kwani kipengele hichi cha matangazo kitaanza kutumika kabisa mwakani, pengine mpaka kikiwasili ndio tutajua haswa.
Kwa haraka haraka ni kwamba mfumo mzima wa matangazo hapa utawekwa wazi na itajulikana dhahiri juu ya namna matangazo haya yatakavyo endeshwa.
Mpaka sasa kinachojulikana kwa asilimia mia ni kwamba huduma hii ya matangazo itakua na gharama ndogo (nafuu) ya vifurushi ukilinganisha na vifurushi vingine ambavyo havitaruhusu matangazo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment je hii umeipokeaje? Je unadhani ni sawa kwa kampuni kuja na kifurushi cha aina hii?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.