Snapchat ni moja ya mitandao ya kijamii ambao wengi waitumia Snapchat asilimia kubwa ni Wamarekani kundi la vijana na kama ilivyo kwa mitandao ya kijamii mingine uraibu wa matumizi upo njenje.
Snapchat imekuwepo kwenye ushindani kwa miaka kadhaa sasa imekuwa ikifanyiwa ikifanyiwa maboresho ili kuifanya kuendana na kile ambacho watumiaji wanakihitaji. Katika maboresho ambayo Snapchat wametangaza hivi karibuni ni uwezo wa kuweza kusambaza kwa rafiki zako mahali ulpo kwa wakati huo kwa ambapo marafiki/jamaa au watu wako wa karibu wanaweza kujua sehemu ulipo kwa muda fulani.
Watumiaji wa Snapchat sasa wanaweza kuwaambia marafiki zao mahali walipo kwa wakati huo (Live location) ambayo wanaweza kuruhusu kitu hicho kidumu kwa dakika 15 au saa kadhaa. Hata hivyo, inawezekana kusambaza kwa marafiki mnaoendana (mutual friends).
Katika kuhakikisha watumiaji wa Snapchat wanapunguziwa hatari ya kuona kama unafuatiliwa au kuombwa na marafiki zako kila mara kutaka wajue mahali alipo inawezekana kusimamisha kusambaza sehemu ulipo bila ya kupeleka taarifa fupi upande wa pili; yaani unaigadisha sehemu mubashara bila yule anayekufuatilia kujua wewe huku umesimamisha vitu 😀 😀 😆 😆 .
Kuruhusu kipengele hiki mtumiaji anatakiwa kwenda kwenye ukurasa wa rafiki yake kwenye Snapchat kisha kuchagua ni kwa muda gani atapenda rafiki yake aje mahali yeye alipo na kipengele hiki kinaonekana tu kwenye uwanja wa kuandikiana jumbe za maandishi.
Hadi sasa kipengele hicho kimepata umaarufu wake na wanaotumia Snap Map wanafikia 250 milioni kwa mwezi. Haya sasa habari ndio hiyo na Snapchat inazidi kuboreshwa. Swali ni je, nani ungependa afahamu mahali ulipo kupitia Snapchat?
Vyanzo: The Verge, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.