Twitter ina watumiaji wengi tuu ambao kwao ni mtandao wa kijamii muhimu sana kuzidi mingine. Umaarufu wake si mkubwa lakini umetokea kuwavutia watu mbalimbali ulimwenguni kote.
Twitter imekuwa katika maboresho mbalimbali ili tuu kuendana na sera za mpya za Umoja wa Ulaya namna ambavyo makampuni makubwa yanakusanya na kuzihifadhi data za watu. Hilo halijaifanya Twitter kuendelea kufanya maboresho kwenye mtandao huo wa kijamii ambapo hivi karibuni tulisikia kuhusu uwezekano wa kuandika “Makala” kwenye Twitter.
Katika kufanya mtandao huo wa kijamii watumiaji wake waweze kuwasiliana kirahisi kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi maarufu “DM” kwa lugha ya Kiingereza. Sasa mtumiaji wa Twitter iwe kwenye kompyuta au simu janja inayotumia Android/iOS ana uwezo wa “Kuwasogeza karibu” hadi watu sita (6) ndani ya ukurasa wake ambapo jumbe zinatunzwa.
Keep your fave DM convos easily accessible by pinning them! You can now pin up to six conversations that will stay at the top of your DM inbox.
Available on Android, iOS, and web. pic.twitter.com/kIjlzf9XLJ
— Twitter Support (@TwitterSupport) February 17, 2022
Kitu hiki Twitter walikisema mwezi Disemba mwaka jana na sasa inaonekana wametimiza lakini bado kuna mengi yanatakiwa kuboreshwa ili kuvutia uwanja ule ambao jumbe zote zinatumwa/kupokelewa zinakuwepo. Hivyo, ni wazi Twitter wataendelea kuleta vitu vipya kwenye mtandao huo wa kijamii.
Vipi msomaji wetu una akaunti ya Twitter? Ni mara ngapi unaperuzi/kuwasiliana na angalau watu sita kwenye mtandao huo wa kijamii wenye umaarufu wake lakini usiovuma kwa sana?
Vyanzo: Twitter, GSMArena
No Comment! Be the first one.