Mtandao wa kijamii wa Twitter unafahamika vyema kwa kuruhusu watu kuandika kitu kisichozidi idadi fulani ya maneno (pamoja na alama za uandishi) lakini hilo sasa huenda likabadilika na kuruhusu watu kuchapisha kitu katika urefu zaidi (kama makala).
Hivi sasa Twitter inaboreshwa na kuongeza kipengele kipya cha “Twitter Articles” ama “Makala za Twitter” kwa mujibu wa tafsiri isiyo rasmi. Kitu hicho ambacho kwa lugha nyingine ni kwamba kitawezesha watumiaji wa Twitter kuweza kuchapisha kitu ambacho kinazidi maneno 280 (zikiwemo alama za uandishi) ambacho ndio kiwango cha juu kabisa cha chapisho kwenye Twitter.
Kupitia akanti ya Twitter ya Bi. Jane Manchun Wong ameweka kiambatanishi ambacgo kinasomeka “No Twitter articles yet” kwa maana yake bado hakula makala ya Twitter halafu chini yake kuna kitufe kilichoandikwa “Create a Twitter Article” ikimaanisha mtu abofye ili aweze kuandika makala kwenye Twitter.
Katika kufanya kitu ambacho kinaendana na hicho ambacho kinatengenezwa kwa sasa nwezi Novemba 2021, Twitter ilileta kipengele kipya cha “Reader Feature” ambacho kinarahisisha usomaji wa machapisho mbalimbali kwa urahisi kwenye mtandao huo wa kijamii-Twitter Blue unaopatikana kwa kulipia ada fulani kila mwezi.
Haijafamika ni lini kipengele hicho kipya kitakuwa na ukomo wa idadi ngapi ya maneno na alama za uandishi lakini hakika zitazidi 280 za sasa. Hata hivyo, ni uamuzi mzuri walioufanya Twitter kuweza kuruhusu watuaji wake kuchapisha kitu kirefu kidogo.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.