WhatsApp programu tumishi inayotumiwa na watu wengi zaidi duniani kama njia ya kufanya mawasiliano kila mara inaboreshwa na sasa umesikia hii ya uwezekano wa kuhamisha mazungumzo yako kwenda namba nyingine?
WHatsApp ambayo haikuwa maarufu kama ilivyo hivi leo zaidi ya miaka kumi iliyopita na tangu ianze kuapata maboresho haijarudi nyuma. Kuna wale ambao tuna akaunti mbili za WhatsApp kwa maana ya kwamba namba mbili tofauti zote zikiwa zinapatikana kwenye programu tumisihi husika.
Katika maboresho ambayo yanapikwa ndani ya WhatsApp ni uwezekano wa kuhamisha mazungumzo yako kutoka namba moja hadi nyingine. Mfano una mpango wa kubadilisha namba kwenye WhatsApp kutoka moja hadi nyingine sasa kabla ya kufanya zoezi hilo unaamua kuhamisha mazungumzo yako na watu ndani ya WhatsApp kwenda kwenye namba nyingine utakayoiweka.
Maboresho hayo ambayo ni dhahiri shairi kuwa yatanzia kwa watumiaji wa Android inawezekana habari hii ikapokelewa vizuri sana hasa ukizingatia kile kinachotokea mara baada ya mhusika kubadilisha namba ya kwenye WhatsApp.
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika yanafanyika majaribio ya kuhamisha mazungumzo ndani ya WhatsApp kutoka kwenye iOS kwenda Android ama Android kuja iOS. Kilichobaki ni kusubiri kuona maboresho hayo yataletwa kwa wote ama la!
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.