Nchini Tanzania suala la usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole si jambo la hiari bali ni lazima.
Usajili wa laini kwa alama za vidole ambao unaenda sambamba na mtu kuwa namba za NIDA ambazo zinamwzesha mtumiaji kuweza kutambulika katika mfumo wa kielektroniki kuwa huyo aliyesajili ndio mmiliki halali wa kadi ya simu fulani, hii yote ni katika kuhakikishausalama na njia mojawapo ya kukabiliana na uhalifu wa mitandaoni.
Kuna kitu ambacho nimepata kukifahamu kwamba usajili wa kadi ya simu za Vodacom Tanzania ni kila baada ya dakika 30 kwa namba husika ya NIDA. Yaani wewe kama unataka kusajili laini ya Vodacom Tanzania zaidi ya moja kwa kutumia kitambulisho hichocho zoezi hilo halitafanikiwa papo kwa papo bali mhusika analazimika kusubiri kwa muda wa nusu saa ili kuweza kusajili laini nyingine ya Vodacom.
Katika hilo kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) hadi sasa watu walisajili kadi zao za simu kwa kutumia mfumo mpya wanazidi ya milioni 28 tu.
Tunashauri kujiepusha kumsajilia mtu kadi ya simu pasipo kuwepo sababu ya msingi kinachokusuma kufanya hivyo kwani utakuja kutafitwa iwapo uliyemsaidia atafanya uhalifu, utapeli, n.k hivyo kuwa makini.
Vyanzo: TCRA, IRM
No Comment! Be the first one.