Suala la Samsung kujenga kiwanda cha vipuri mama huko Austin-Texas, Marekani sasa limrasimishwa na ujenzi huo utaanza mwaka 2022.
Kurasimishwa kwa jambo hilo kunafuatia baada ya viongozi wa pande mbili kwa maana ya serikali ya jimbo la Texas na Makamu wa Mwenyekiti wa Samsung, Bw. Kinam Kim kukutana na waandishi wa habari na kuliweka wazi suala hilo huku ujenzi huo ukitarajiwa kuanza mwaka 2022 na utengenezaji wa vipuri mama kuanza mwaka 2024.
Kipi kilichosukuma ujenzi wa kiwanda hicho?
Samsung wamevutiwa kujenga kiwanda hicho nje kidogo ya Austin-Texas kwa sababu kadhaa na baddhi yake zikiwa ni “Msamaha wa aina fulani” kwa lengo la kuvutia wawekezaji lakini pia utayari wa viongozi wa eneo husika kuwa wepesi kukaribisha ujenzi wa kiwanda hicho halikadhalika utulivu wa miundombinu ya eneo husika. Vilevile, hivi sasa dunia inakabiliana na changamoto ya uhaba wa vipuri mama ambavyo vinatumika kwenye vifaa mbalimbali kama simu, teknolojia ya utashi usio halisi. Hivyo, kwa ujenzi wa kiwanda hicho maana yake kitapunguza changamoto hiyo ambayo inaitesa dunia hivi sasa.
Faida za kiwanda cha vipuri mama cha Samsung
ujenzi wa kiwanda hicho unatajwa kugharimu zaidi ya $17 bilioni ambapo utaanza mwaka 2022 na ukitarajiwa kukamilika miaka miwili baadae (2024). Kiwanda hicho kinatazamiwa kuzalisha karibu ajira 2000 kwenye upande wa utengenezaji wa teknolojia ya 5G, vifaa vya kutumika kwenye kompyuta za hali ya juu halikadhalika utashi usio halisi (AI).
Kufuatia janga la virusi CORONA ambalo bado linaendelea kuitafuna dunia makampuni mengi ambayo yanajihusisha na utengenezaji vipuri kwa ajili ya magari yanayoweza kujiendesha yenyewe sasa yanabadilisha upepo na kuanzisha viwanda vya kutengenza magemu yaliyo katika mtindo wa picha jongefu (“Video“).
Vyanzo: GSMArena, NPR
No Comment! Be the first one.