Kwenye ulimwengu wa simu janja masasisho ni kitu muhimu sana ambacho kinasaidia kufanya rununu kuwa katika ufanisi lakini pia kuondoa kasoro ambazo zinaweza kusababisha kifaa husika kudukuliwa.
Samsung ina mtindo wa kutoa upendeleo wa aina yake kwa baadhi ya simu janja zake tofauti na nyinginezo yaani kwa kumaaanisha unakuta toleo la simu ni lilelile lakini limegawanywa katika makundi mawili tofauti. Simu nyingi za Samsung huko ughaibuni zipo katika kundi hili la wengi na nyingine ni zile zilizopewa hadhi fulani ambapo kwa lugha rahisi zipo upande wa “Enterprise“.
Ni kawaida sana kwa simu janja za Samsung zilizo katika kundi la “Enterprise” kupewa muda mrefu wa kupokea masasisho mbalimbali kulinganisha na hizi nyinginezo. Sasa zile ambazo zipo kwenye kapu la “Enterprise” limehakikishiwa kupokea masasisho kwa miaka mitano mfululizo tangu kuzinduliwa kwake.
Simu janja ambazo zimepewa upendeleo wa kipekee kupokea masasisho katika kipindi cha miaka mitano ni Galaxy S20, S20+, S20 Ultra, Note20, Note20 Ultra, XCover 5 na Galaxy Tab Active 3.
Mara nyingi tuu Samsung huruhusu masasisho kwenda kwenye rununu ilizozitengeneza kwa miaka minne mfululizo na upendeleo wa aina yake kwa baadhi ya bidhaa kama hizo zilizotajwa hapo juu.
Je, wewe unamiliki simu janja iliyopewa upendeleo wa kupokea masasisho kwa muda wa miaka mitano?
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.