Kampuni ya Apple inayohusika na uundaji pamoja na utengenezaji wa simu janja za iPhone imepanga kuanza kutengeneza modem zake wenyewe za 5G kwaajili iPhone zitakazoanza kutoka mwaka 2023. Apple pamoja na makampuni mengine ya utengenezaji wa simu hutumia modem za Qualcomm kwaajili ya mtandao katika simu janja zake.
iPhone zilizotoka mwaka 2021 zinatumia chipu ya Qualcomm X60 na zile zinazotarajiwa kutoka mwaka 2022 zitatumia chipu ya Qualcomm X65. Ili kufanikisha lengo lake la kutengeneza chipu za 5G kampuni ya Apple itashirikiana na Taiwan Semiconductor Manufacturing Co (TSMC). Katika ushirikiano huu Apple imepanga kutumia chipu aina ya TSMC 4nm ambazo bado hazijaanza kutumika katika simu janja yoyote.
TSMC imekuwa na ushirikiano mzuri sana na Apple katika siku za hivi karibuni na imekuwa na jukumu la utengenezaji wa vichakataji vyote vya iPhone na pia mifumo ya M1 kwenye chip kwa kompyuta za Mac. Kampuni hii ilionyesha umahiri wake baada ya kufanikiwa kuitengenezea Apple chipu ndogo sana kwa ajili ya simu janja zake.
Je, una lipi la kusema kuhusiana na habari hii? Tupe maoni yako na daima teknoKona tunapenda kusikia maoni ya wasomaji wetu kutoka kila pembe ya dunia.
Soma zaidi kuhusu makala hii hapa. Endelea kutembelea tovuti yetu uweze kujifunza zaidi kuhusu teknolojia na matumizi yake. Soma makala zetu zingine hapa.
Vyanzo: Techbooky, GSMArena
No Comment! Be the first one.