Watumiaji wa WhatsApp wengi tunafahamu kuwa hivi sasa tunaweza kuonyesha hisia zetu kwenye jumbe ambazo tunazipokea iwe kutoka kwa mtu mmoja mmoja au kikundi.
Miezi miwili baadae baada ya kipengele cha kuweza kuonyesha hisia zetu kwenye jumbe zwa WhatsApp kwa kutumia vikatuni (emoji) iimeonekana maboresho yanahitajika kukifanya kitu hicho kivutie zaidi. Fahamu ya kuwa WhatsApp wanaboresha kipengele hicho kiasi cha kuweza idadi ya wangapi wamependa, kuchukizwa, kuhuzunishwa, n.k kulingana na ujumbe walioupokea.
Hii maana yake ni kwamba mtu (mhusika) aliytuma ujumbe kwenye WhatsApp ataweza kujua ni wangapi wameweza kupenda, kucheka, kulia kulingana na kile ambacho ametuma kwenda kwa mtu mwingine au kundi/makundi.
Kipengele hicho ambacho hivi sasa bado kipo kwenye hatua ya matengenezo lakini inaonekana kinafanyika na kama mabo yalivyo kwenye Facebook, Instagram, Linkedin pamoja na mitandao mingine ya kijamii.
Swali la msingi je, ni lini maboresho hayo yataanza kupatikana? Jibu swali la swali ni kwamba bado haijulikani lakini kama kimenaswa na WaBetaInfo basi hakika lisemwalo lipo hivyo endelea ktufuatilia na tutazidi kuwahabarisha kuhusiana na kuweza idadi ya watu walioonyesha hisia zao kwenye ujumbe husika ndani ya WhatsApp.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.