Samsung wameendeleza wimbi la kutoa simu janja na safari hii bado wameangazia wale watu ambao hawana uwezo wa kununua rununu ghali lakini wanapenda kuendana na teknolojia hapo ndipo tunakutana na Galaxy A03 Core.
Kwenye ulingo wa simu janja Samsung wanajiweka sawa kila uchwao kwa kuendelea kutoa simu janja ambazo zitapata soko na hatimae kuiingizia faida kampuni halikadhalika kuendelea kuleta ushindani kwa wapinzani wake. Jicho la TeknoKona limeona ni vyema kuileta Samsung Galaxy A03 Core mbele ya wasomaji wake ambayo ina sifa zifuatazo:-
Kwanza kabisa munekano wa simu hii ni wa kioo chenye urefu wa inchi 6.5, ung’avu wake ni wa hali ya juu vilevile kamera yake ya mbele ambayo ina MP 5 imeingia kwa ndani kidogo na kutengeneza umbo sawa na tone la maji.
Pili, kwa upande wa memori na kamera Samsung Galaxy 03 Core imewezeshwa na GB 2 za RAM, 32 GB-diski uhifadhi lakini pia ipo nafasi ya kuweka memori ya ziada. Upande wa nyuma una kamera moja tu ambayo ina MP 8+taa ya kuongeza mwanga sehemu hafifu.
Tatu, betri ya kwenye simu hii ina 5000mAh na ina teknolojia ya kuchaji haraka kwa nguvu inayofikia 10W, ipo katika toleo mbili tofauti; moja ni zile ambazo zinatuma kadi moja tu ya simu huku kuna nyingine zina uwezo wa kuweka kadi mbili za simu kuwezesha kupiga/kupokea simu.
Hadi wakati makala hii inaandaliwa bei ya simu husika ilikuwa haijafahamika lakini inatazamiwa kuingia sokoni mwezi Disemba.
Jicho la TeknoKona linahitimisha kwa kusema kuwa hii ni simu janja ya uwezo wa kawaida kabisa na haina mambo mengi kuweza kuifanya iwe na mvuto wa aina yake lakini inafaa kwa matumizi ya kawaida.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.