Apple kwa sasa wanatamba na toleo jipya la simu janja ambalo zilizinduliwa Septemba 14 ya mwaka huu kama ilivyo kawaida yao. Lakini kuna uhaba wa iPhone 13 ambao umeikumbuka kampuni husika na hali hiyo inatazamiwa kuendelea hadi Februari 2022.
Nchi nyingi tuu hivi sasa iPhone 13 hazipatikani na hii inatokana na uhaba wa vipuri mama ama kwa lugha iliyozoeleka ingawa si rasmi tunasema “Prosesa”. Apple wamejitahidi kutunza fedha kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa vipuri mama ambavyo vinatumika kutengenza iPhone lakini hali bado ni ngumu.
Yapo makampuni kama TSMC yamehifadhi vipuri ulizajishaji wa vipuri mama kwa ajili ya iPhone 13 lakini bado inaonekana kuwepo kwa changamoto ya kuweza kukabiliana na mahitaji ya soko.
Uhaba huu kwa hakika hata ambazo zinapatikana kwa sasa kuuzwa ghali zaidi kwani waswahili waliwahi kusema “Kufa kufaana” na kwa upande mmoja ni tatizo lakini ukipindua shilingi imekuwa kama fursa kwa wafanyabiashara kupata faida zaidi kutokana na hali ambayo mataifa mengi yanavyokabiliana na uhaba wa iPhone 13 sokoni.
Taarifa zilizopo hali hii itaendelea hadi Februari 2022 hivyo basi ni wakati sasa wa wapenzi wa iPhone kufikiria cha kufanya kama ni kununua toleo la juu ama kuendelea kuwa mvumilivu hadi mwakani.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment