Vifaa vyetu vya kidijiti vimekuwa vikitusaidia sana na hata kwa kiasi fulani kutumia sauti tu kama amri kutaka kitu fulani kifanyike. Nikisema “Google Assistant” wengi mnaifahamu lakini sasa programu inatazamiwa kutanua wigo wake.
Kama ni mtu unayependa kutumia mbinu mbadala pasi na shaka utakuwa umetumia programu ya usaidizi kutoka Google mara kadhaa kama njia mojawapo ya kutaka jambo fulani lifanyike kwenye simu janja.
Google wanataka kufikisha watumiaji bilioni moja ambao wanatumia programu ya usaidizi kutoka kwao na safari hii simu za kawaida zikiwa ndani ya mpango huo; yaani kuweza kutumia sauti kuamuru kitu fulani kifanyike hata kwenye rununu zisizo simu janja.
Google Assistant ipo zaidi kwenye simu janja za Android lakini kwa mujibu wa Amazon walionunua Alexa kutoka kwao mpaka sasa idadi yao imefikia milioni 900 na Google wanatarajia kufikia vifaa vya kidijiti bilioni moja hadi kufikia mwisho wa mwezi Januari 2019.
Vipi wewe ni mmoja wa watu ambao hupendelea kutumia programu ya usaidizi kutoka Google? Au ulikuwa hujui hata kama ipo? 😆 😆 . Usione aibu kusema ukweli.
Vyanzo: The Verge, Android Community