Uvaaji wa saa janja umekuwa ukikua mwaka hadi mwaka na makampuni mbalimbali yamekuwa yakitoa kifaa hicho cha kuvaa mkononi pamoja na masashisho ambayo zinafanya ziwe imara kuziepusha na mabaya kwenye ulimwengu huu wa teknolojia.
Wakati Samsung inafanya uzinduzi mkuwa wa simu janja-Galaxy S21 na tabiti-Galaxy Tab S8 iliweka wazi vitu muhimu pamoja na kusema imeboresha sera zake ikiwemo kipengele cha kupeleka masasisho rununu ambazo inazitengeza kuanzia zilizotoka muda kidogo, za mwaka huu na zitakazokuja. Samsung imeweka wazi kuwa bidhaa hizi zitapokea masasisho ya programu endeshi katika kipindi cha miaka minne (4) na miaka mitano ijayo kuanzia mwaka huu ikihusisha masasisho mengineyo.
Moja ya bidhaa hizo ambazo zimeingia kwenye mpango wa miaka minne ya kupokea masasisho ya programu endeshi na miaka mitano ya masasisho yanayohusu kukifanya kifaa husika kiwe salama zaidi ni saa janja-Galaxy Watch 4 kwenda mbele. Mpango huo unajumuisha Galaxy Watch 4, Galaxy Watch 4 Classic pamoja na nyinginezo ambazo zitatoka huko mbeleni.
Hivi karibu Samsung imepeleka masasisho makubwa kwenye saa janja za toleo la nne la familia ya Galaxy Watch ambpo kuna mengi yaliyoboreshwa na kufanya zizidi kuvutia.
Kimsingi kupakua masasisho ni kitu muhimu kwa usalama wa vifaa vyetu vya kidijiti. Hivyo, hatupaswi kupuuzia pale taarifa fupi inapokuja iwe kwenye simu/saa janja-Galaxy Watch 4 au nyinginezo.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.