Katika ulimwengu wa “Kileo” watu wengi duniani wana akaunti Instagram ambayo imekuwa kivutio cha cha watu duniani kote na hata kusababisha uraibu. Sasa wamezindua “Reels“.
Uweo wa kupakia picha jongefu ambazo si ndefu (kati ya sekunde 15 hadi 60) zimekuwa kivutio cha wengi ambapo hivi sasa TikTok ipo katika umaarufu wake na hata kupatikana katika nchi takribani 50 duniani kote. Instagram nao wakaona kuna haja ya kuleta mpinzani waliyemuita “Reels“.
Kipengele hiki kipya kinapatikana ndani ya Instagram kwenye kitufe cha kamera kilichopo upande wa kushoto juu ambapo mtumiaji anaweza akarekodi picha mnato ya urefu wa sekunde 15, kuweza kuiwekea ujumbe wa sauti pamoja na nakshi nakshi nyningine nyingi tuu kisha kuipeleka hewani kwa watu kuweza kuitazama.
Upo uwezekano pia wa kuitunza kwa muda fulani kwa lengo la kutaka kufanyia maboresho kadha wa kadha kabla ya kuiruhusu kwenda hewani, kuweza kubadilisha picha ya ukurasa (cover photo). Machapisho yote ya “Reels” yanaonekana kwenye kipengele cha “Feed” au “Discover tab“.
Unajiuliza kama kimeshawafikia watumiaji wa Instagram bara la Afrika? Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali nchi ambazo kipengele hicho kimeshafika ni Marekani, Uingereza, Ufaransa, Japan, Brazil, Australia, Ujerumani na India.
Vyanzo: The Verge, GSMArena
One Comment
Comments are closed.