Mfumo wa kutumia jumbe za sauti kueleza kitu fulani na ta kuwasambazia wengine kwenye WhatsApp na kwingineko imekuwa ni kitu cha kawaida sana na watu wengu wanatumia duniani kote.
Mfumo huu wa kutumia sauti kupekeka ujumbe kwa mtu mwingine ndani ya WhatsApp umekuwa msaada mkubwa kwa watu wengi hasa pale ambapo mtu anataka kujibu kitu kwa haraka zaidi pengine hata kutoa maelezo ya kina kuhusiana na ujumbe anaotaka kupeleka.
Maraa kadhaa mfumo wa kutumia jumbe za sauti umekuwa ukiboreshwa na kufanya kuwa na kitu kipya kinachokwenda kubadilisha mtindo wa watu waninavyotumia; ukisema uwezo wa kusimamisha/kuendelea kurekodi, kuweza kupeleka haraka haraka/polepole wakati wa kusikiliza, n.k. Sasa kuna mengine mapya ambayo ni:
Rangi ya kuonyesha ujumbe huu “Umesogezwa” (forwarded)
WhatsApp wanaleta mabadiliko ya rangi kwa jumbe za sauti ambazo ametumiwa mtu zaidi ya mmoja ambapo rangi ya Machungwa (badala ya rangi ya njano iliyotumika awali). Halikadhalika, tofauti ya alama zinazotumika kuashiria huu ni ujumbe wasauti uliorekodiwa kwenye WhatsApp na aina nyingine ya ujumbe ulio katika mfumo wa sauti. Pia, ujumbe wa sauti ambao umerekodiwa kwenye WhatsApp na kusambazwa kwa wengi utaonyesha alama ya mawimbi mawimbi iwapo tu wakati ambao ulipokuwa unaandaliwa aliyeurekodi alikuwa anatumia toleo la WhatsApp ambalo kipengele hicho kilikuwa kimesharuhusiwa.
Mabadiliko hayo yameonekana kwa watu wachache sana tena walipo kwenye programu ya WhatsApp toleo la majaribio kwenye upande wa Android. Kitu cha kufanya ni kuhakikisha unapakua masasisho kila mara yanapokuwepo ili kuweza kuona yaliyoboreshwa kwenye WhatsApp.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.