Apple bado inaendelea kuwa kwenye vichwa vya habari kutokana na bidhaa zake zilizozinduliwa mapema mwezi Sept. 2018 kuonekana kuwa si shwari.
Yapo mengi sana yanayozungumzwa kuhusiana na simu rununu ambazo Apple walizitambulishwa kwa ulimwengu Sept. 12 lakini sasa baadhi ya iPhone XS na XS Max zimebainishwa na waliozinunua kuwa na shida upande wa kuchaji.
Tatizo lenywe ni kutokubali kuchaji iwapo haitoi mwanga (kioo kinakuwa kimezima); tatizo hilo ni kwenye kimemeshi cha iPhone XS na XS Max.
Ili kuweza kufanya simu hizo kuchaji basi inabidi zinawaka (mwanga ukionekana kwenye kioo) kisha kuchomoa na kuchoka tena kimemeshi.
Shida yaonekana kwenye baadhi ya iPhone XS na XS Max.
Apple wamekuwa kimya kuzungumzia suala hilo ingawa upande wa teknolojia ya kuchaji bila kutumia waya hauna shida.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|