Mara kwa mara WhatsApp imekuwa ikifanyiwa maboresho ambayo yanaifanya programu tumishi husika kuweza kuvutia kinamna yake na kuna kitu kingine kipya; kinahusu uwezo wa kuangalia picha/video mara moja tu.
Katika pitapita zangu za huku na kule nikakutana na habari ambayo imenivutia kuhusu WhatsApp; kuna maboresho yanafanyika ambapo mtu ataweza kuona picha/picha mnato iliyotumwa mara moja tu! Inakuaje hii?
Mapema mwezi Juni kipengele hicho kiliwekwa kwenye majaribio na baada ya muda fulani kikaondolewa lakini sasa huenda watumiaji wa WhatsApp wakaweza kuona kipengele hicho kipya.
Inakuaje?
Inaelezwa kuwa mtumiaji wa WhatsApp ambae ameruhusu kipengele hicho kipya akishatuma picha/picha mnato kisha yule aliyepokea akakufungua kuangalia na kufunga picha kitu hicho kitatoweka mara moja!
Kuna watu wanaweza kuwa wepwesi wa kuweza kunakili kitu husika kwa “Kukipiga picha ya papo kwa papo” (screenshot) ama kurekodi kabla ya kufunga kitu husika. Basi fahamu ya kuwa iwapo utakumbuka kufanya hivyo WhatsApp haitapeleka taarifa kwa aliyetuma kuwa picha/video imeshanakiliwa/kurekodiwa kutokana na kwamba inatumwa katika mtindo wa usiri kati ya pande mbili husika (end-to-end encryption).
Haya sasa mdau wa TeknoKona tuambie unakizungumziaje kipengele hiki ambacho tutakiona katika siku za usoni? Je, ni kizuri au kibaya kwenye WhatsApp? Tunakaribisha maoni yako.
Vyanzo: GSMArena, Engadget
No Comment! Be the first one.