Kwa watumaiaji wa mtandao wa WhatsApp kuna njia mbalimbali ambazo ziko kama viashiria kwamba mtu ameku’block katika mtandao wa huo.
Ni sawa viashiria hivi havina ushahidi wa asilimia mia kabisa kwamba ume’block’iwa lakini ni moja ya namna ya kujua- sijui kama naeleweka!
Kumbuka mtandao wa WhatsApp haukutaarifu moja kwa moja kama ume’block’iwa hivyo basi inakubidi tuu kutumia njia mbadala ili kujua hivyo.
Viashiria Hivyo Ni Kama Ifuatavyo!
- Angalia Last Seen au Online Status
Kama unahisi mtu amekublock kwa haraka haraka angalia kama unaweza kuona status zake (kama anapost) na pia angalia ‘last seen’ yake. lakini hapa kumbuka kama atakua amezima (kuamuru kutoonesha) kupitia settings basi hutaweza kuona.
- Angalia Katika Profile
Kaa ukijua kama mtu amekublock katika mtandao wa WhatsApp kamwe huwezi kuona picha yake katika profile. Hutoweza kuona hata kama akibadilisha tena picha.
- Jaribu Kumtumia Meseji
Hapa hata ukituma meseji kama mtu ameku’block basi kaa ukijua kwake itamfikia meseji ambayo imepiga tiki moja tuu. Hii ni tofauti maana kwa mtu ambae hajaku’block kwa kawaida meseji zinaanza kupiga tiki moja alafu zinafuata kuwa mbili.
- Jaribu Kumpigia Simu (Kwa Kutumia App Ya WhatsApp)
Kama amekulamba block kaa ukijua hata ukijaribu kumpigia simu basi simu hiyo haitatoka (haitomfikia). Utaona tuu ujumbe unaosema ‘Calling’ lakini hutoona simu hiyo ikiandika ‘Ringing’ au ikipokelewa.
- Jiunge Group Moja Na Unaehisi Ameku’Block
Kama utaunga group lako na mtu ambae unahisi ameku’block, ukisha maliza utashangaa ndani ya ‘group’ uko mwenyewe.
Hivyo ni baadhi ya viashiria vinavyoonyesha kuwa mtu amekublock katika mtandao wa WhatsApp. Kama unahisi kuna mtu amekublock basi fuatulia mbinu katika vipengele vyote ili kuwa na uhakika zaidi.
No Comment! Be the first one.