Matoleo ya Android 2.3.7 na ya zamani zaidi hayataweza kuingia katika akaunti za google. Hii inamaana kuwa kama ana kifaa cha Android ambacho kina toleo hilo ….
Au la nyuma zaidi basi haitawezekana kabisa kuingia na akaunti yako ya Google katika kifaa hicho. Android 2.3.7 kwa jina lingine linajulikana kama Gingerbread (tena lile toleo la mwisho la toleo hilo).
Sasa Google wametoa tarehe ambayo itaachana kabisa na matoleo hayo na tarehe hiyo ni septemba 27. Sababu kuu kwao Google wanasema kwamba….
Wanafanya yote hayo ili kuhakikisha kwamba watumaiji wa vifaa ba bidhaa zao wanakuwa salama wakati wanatumia huduma na bidhaa zao.
Baada ya tarehe hiyo unaweza ukawa unaingia katika akaunti hiyo kupitia kifaa chenye toleo la Gingerbread au la zamani zaidi usije ukashangaa unaambiwa nywila yako au taarifa zako hizo sio sahahi.
Hili sio la kushangaza sana kwani kama una kumbukumbu vizuri ni kwamba toleo la Gingerbread limetokea takribani miaka kumi iliyopita.
Vifaa ambavyo vinatumia Android 3.0 (Honeycomb) na kuendelea vitakua salama kabisa maana havitakua na zuizi la aina yeyote.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment hii umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.