Hapa ni kwamba kuna habari zilikua zinasambaa chini chini kwamba bilionea wa marekani Elon Musk ana mpango wa kuchukua cheo cha mkurugenzi mkuu kwenye kampuni ya Apple.
Kinachofahamika kwa sasa ni kwamba mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Apple ni bwana Tim Cook ambaye alirithi mikoba kutoka kwa Steve Jobs.
Kingine ambacho labda kimefanya fununu hizi kusambaa sana ni sababu ya umahiri ambao anao bwana Elon katika utendaji wake wa kazi, ni wazi anasimamia makampuni mengi sana moja wapo kati ya kampuni hizo ikiwa ni ile ya Tesla.
Ni wazi tangia awe mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Tesla, kampuni iliongezeka thamani yake na yeye mwenyewe binafsi kujipatia utajiri mkubwa ambao umemfanya aingie katika chati ya juu kabisa ya mabilionea duniani.
Sasa basi wenyewe wawili ,Tim Cook Wa Apple na Elon Musk Wa Teslsa, Wanasemaje?
Hapa viongozi wote hao wawili wamekanusha kabisa hizo na kwamba hata wao wawili hao kuongea tuu haijawahi tokea ingawa Elon Musk alishawahi kumuandikia Tim Cook ile kama kuna uwezekano Apple inunue Tesla ila ikashindikana.
Cook & I have never spoken or written to each other ever.
There was a point where I requested to meet with Cook to talk about Apple buying Tesla. There were no conditions of acquisition proposed whatsoever.
He refused to meet. Tesla was worth about 6% of today’s value.
— Elon Musk (@elonmusk) July 30, 2021
No Comment! Be the first one.