Facebook licha ya kuwa moja ya mtandao wa kijamii mkubwa na mkongwe sana kwa muda mrefu umekua ukipambana katika kuhakikisha inakuja na bidhaa ambayo inashikika.
Ni kweli tunjaua kuwa Facebook huwa haifanyagi vizuri sana katika aina hizi za bidhaa… licha ya kusema haya unaweza ukashangaa labda pengine ni sababu hawajapata ile bidhaa (umeelewa sio?)

Mkurugenzi mkuu wa Facebook, Mark Zuckerberg amethibitisha kuwa miwani hizi zinakuja na mtengenezaji ni kampuni maarufu kabisa ya miwani (inaweza kuwa ni kampuni maarufu zaidi katika bidhaa hiyo)
Unaweza ukaanza jiuliza kuwa bidhaa hii itaanza patikana lini, Facebook hawakuongelea juu ya hili lakini fununu nyingi zinasema kuwa bidhaa hii itapatikana muda wowote mwaka huu.
Lakini kwa sasa kwa mtazamo wangu ni kwamba makampuni mengi huwa yanabadilisha ratiba zao kwa kiasi kikubwa sababu ya gonjwa la CORONA.
Kingine cha kuchekesha ni kwamba facebook imesema miwani miwani hii ni mizuri na ukiwa nayo unaweza ukafanya vitu vizuri (nadhifu) lakini ni kwamba hawajasema vitu hivyo.

Miwani janja hii itakua ni ya kwanza kabisa kutoka kampuni ya Ray-ban na watakua wanashirikiana na kampuni ya EssilorLuxottica.
Kwa haraka haraka mimi binafsi ninavyofikiri ni kwamba miwani hiyo (nadhani) kwa kiasi kikubwa itakua inahusika na mambo ya picha picha na video….
Nahisi unaweza iunganisha na mtandao wao na kuanza kuchukua baadhi ya picha na video ambazo zinaweza zikajipost katika kipengele cha ‘story’ cha Facebook
Kupata ukweli kamili tusubiria taarifa zenye maelezo ya kina kuhusiana na jambo hili kutoka kwao Facebook wenyewe hivyo tuendelee kusubiri.
Picha Zote Na Chapisho Havihusiani Moja Kwa Moja!
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment, Niambia Hii Umeipokeaje?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.