Katika ulimwengu wa simu janja Nokia wamekuwa wakijitahidi kufaya hishima waliyokuwa nayo miaka mingi iliyopita inarudi na kuendelea kuvutia watu wengi zaidi. Ukiongelea bidhaa mpya kutoka HMD Global hivi sasa basi ni Nokia XR20.
Teknolojia imekuwa hivyo mambo mengi yamebadilika kwenye sekta zima ya mawasiliano na simu janja kwa ujumla. Siku hizi ni kawaida kumuona mtu akimaliza kazi nyingi tuu kupitia simu ya kiganjani na hii inatokana na uwezo ambao rununu unakuwa nao kiasi kwamba vifaa kama kompyuta vinakuwa havihitajiki kukamilisha kazi fulani.
Nokia XR20 ni moja ya simu janja ambayo imewezeshwa vitu vingi ambavyo watu wengi tuu duniani kote vinawavutia na hatimae kununua rununu fulani. Bila kuwasahau kuna wale ambao tangu waanze kumiliki simu ya mkononi wameamua kutulia na bidhaa ya kampuni fulani tu. Simu hii ina sifa zifuatazo:-
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.67
- Ubora: IPS LCD (1080*2400px); ung’avu wa hali ya juu sana+ kamera ya mbele ipo katikati ya uso wa mbele
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+sehemu ya kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4/6
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 48 na 13+taa mbili za kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 8+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4630 mAh
- USB-C 3.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 18W, 15W za kuchaji kwa haraka bila kutumia waya
Kipuri mama :
- Snapdragon 480 5G
Uzito :
- Gramu 248
Programu Endeshi
- Android 11
Rangi/Bei :
- Kahawia na Bluu
- GB 4/64-$538 (zaidi ya Tsh. 1,237,400) na GB 6/128-$679 (zaidi ya Tsh. 1,561,700) bei ya ughaibuni
One Comment