Kwa sasa simu janja zipo katika ukubwa wa aina tofauti tofauti. Je, ukubwa wa simu janja una tija kweli au sio kitu cha msingi kama vile kampuni nguli la Nokia linavyosema?
Pengine kwa wengine umbo ni kitu cha muhimu zaidi katika simu. Vipi kuhusu na teknolojia ya ndani ya simu hiyo lakini? Ni jambo la msingi kuwa na teknolojia kubwa ndani ya simu hilo liko wazi.
Kwani umbo ni kitu cha muhimu sana au tunafuata mikumbo tuu? Pengine simu yenye kioo (display) kubwa sio ujinga bali ni matakwa ya mtu. Watu tuna machaguo sio? Pengine matumizi yako na yangu yako ni tofauti.
Mtu unaweza pendelea kutumia simu yenye kioo ndogo kwa sababu labda mahitaji mambo mengi katika simu. Fikiria mtu ambae ana matumizi mengi katika simu kama vile kutazama picha jongefu, kucheza magemu, kutuma barua pepe na mambo mengine mengi ambayo yanaladhimu kuwa na simu yenye kioo kikubwa.
Simu ndogo kwa upande mwengine sio kitu kibaya sana kuwa nacho haswa kwa wale wanaopenda simu ambazo zinakaa vizuri katika mkono. ukiachana na hilo ni kwamba simu janja ndogo ni kwamba kwa kawaida haziwezi kuwa na vipengele vingi ukilinganisha na simu kubwa.
No Comment! Be the first one.