Dunia nzima bado inapambana na janga la virusi vya Corona ambalo mpaka sasa limeshagharimu mamilioni ya maisha ya watu ulimwenguni kote.
Makampuni mbalimbali duniani yameboresha sera zao kama moja ya kukabiliana na janga la UVIKO-19 ambapo Apple imebadilisha mbinu za kufahamu hali za kiafya za wafanyakazi wao katika suala zima la virusi vya Corona.
Ingawa haijalazimisha lakini Apple imekuwa ikiwasukuma wafanyakazi wake waweze kupata chanjo ya virusi vya Corona ambapo kwa wale ambao hawajachanja na wanatoka na kwenda kuzunguka kwenye maduka ya rejareja basi wao watapimwa mara kwa mara kufahamu iwapo wapo salama dhidi ya UVIKO-19 ama la!.

Facebook, Google pamoja na makampuni mengi makubwa kwenye ulimwengu wa teknolojia haijawabana wafanyakazi wake kuhusu suala zima la chanjo ya virusi vya Corona halikadhalika kwa Apple ingawa wao wameanza kuomba taarifa iwapo wamechanjwa au la tangu Septemba hii ianzie.
Kutoka idara ya wafanyakazi, usalama kazini nchini Marekani hivi karibuni makampuni makubwa yatalazimika kufanya iwe ni lazima kupata taarifa za wafanyakazi wao iwapo wameshachanjwa chanjo ya UVIKO-19 au la! Au iwe inawapima kila wiki. Vipi ewe msomaji wetu mambo yakoje nchini mwako?
Kumbuka kufuatilia TeknoKona ili uweze kuhabarika halikadhalika kuelimika kuhusu teknolojia.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.