Ni ngumu kuamini kuwa kompyuta nayo inaweza kukosea wakati fulani kwani wengi wetu tunaamini kuwa kompyuta ni “Ubongo wenye akili isiyokosea”.
Si sawa kuziamini kompyuta zetu kwa asilimia zote kwani ni dhahiri kuwa kompyuta nayo inaweza ikakosea kwa kutoa jibu lisilosahihi/kufanya kitu tofauti na ilivyoamriwa. Kujua zaidi kuhusu app ya siri ingia-> hapa kupata kuijua app ijulikanayo kama Siri iliyo chini ya kampuni nguli-Apple.

Kukosea kwa app ya app kumejiri baada ya kuulizwa tarehe ya mwisho ya wamarekani kujisajili katika daftari la wapiga kura na app hiyo kujibu kuwa tarehe ya mwisho ya kusajili watu kwa ajili ya uchaguzi imeshapita ilihali tarehe hiyo bado haijapita ila kila jibo ina tarehe tofauti ya kusajili wananchi wake kwa ajili ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi November.
Ili mwananchi wa Marekani (mwenye haki ya kupiga kura) aweze kupiga kura Nov 8 itambidi awe amesajiliwa. Baadhi ya majimbo nchini humo yanaruhusu mtu kujisajili mtandaoni (online).
Mwezi June Apple walitangaza kuwa app hiyo itakuwa kwenye kompyuta aina ya Mac ambazo zinatengenezwa na Apple (kampuni) kitendo ambacho itasaidia watumiaji wa kompyuta aina ya Mac kuiuliza App ya Siri kwa kile wanachokitafuta kwenye kompyuta na kutoa jibu.

Hivi karibu app hiyo ilipouliizwa inajisikiaje kuwa kwenye Mac ilijibu kuna nafasi ya kutosha ingawa hakuna madirisha pia kuta za zake sio za aluminium. Jibu hilo si sahihi kulingana na swali lililokuwa limeulizwa.
2 Comments
Comments are closed.