Akaunti zinazotukana wanamichezo kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram kuchukuliwa hatua hii ikiwa ni pamoja na kufungiwa.
Baada ya malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wanamichezo na vyombo vinavyowawakilisha, kampuni ya Facebook – ambao ni wamiliki wa mtandao wa kijamii wa Instagram wasema wataanza kuchukua hatua kali dhidi ya akaunti zinazotumia mtandao huo wa kijamaa kutukana wanamichezo.
Katika mabadiliko ya sheria au mikataba ya watumiaji wa mtandao huo wa kijamii, Facebook wamesema akaunti zitakazoripotiwa kutuma ujumbe (DM) wa matusi kwa akaunti za wanamichezo zinaweza jikuta kufungiwa kabisa kutoka kwenye huduma ya Instagram.
Katika wiki chache za hivi karibuni wachezaji kama vile Marcus Rashford na Axel Tuanzebe wa Manchester United wamelalamika juu ya kutukanwwa matusi ya kiubaguzi kupitia mtandao huu wa kijamii. Inadaiwa wengi wanapata shida zaidi pale matusi hayo yakitumwa kwa njia za ujumbe wa DM – na sasa Facebook moja kwa moja watachukua hatua kali kwa mtu yeyote ambaye akaunti yake itaripotiwa kutuma ujumbe wa matusi.
No Comment! Be the first one.