Imekuwa desturi ya kampuni nguli na inayofanya vizuri katika biashara ya vifaa vya kieletroniki kuwa wao tu wenye idhini ya kurekebisha simu (iPhone) kutoka kwenye kampuni yao pale ambapo mteja ataileta ili ifanyiwe matengenezo ya kitu fulani lakini hilo sasa lipo mbioni kubadilika 😯 😯 .
Vifaa vya kieletroniki kupata hitilafu si jambo la kushangaza na hivyo basi kuhitaji matengenezo aidha makubwa au madogo kulingana na ukubwa/udogo wa tatizo lenyewe. Hapo awali iwapo simu yako (iPhone) ikipata tatizo na ukaenda kwa fundi kwa ajili ya matengenezo basi ilimbidi fundi huyo achukue simu yako na kuipeleka katika duka la Apple ifanyiwe matengenezo halafu ndio akurudishie.
Apple sasa imeamua kuacha kuwa yeye tu kuwa na uwezo wa kurekebisha simu zake. Mashine zao spesheli (iPhone calibration machine) zinazotumika katika kufanikisha iPhone 6s na matoleo yaliyofuata baada ya iPhone 6s zimetolewa kwa kampuni 3 zilizoidhinishwa kuwa na uwezo wa kufanya matengenezo kwa simu kutoka Apple.
Soma pia: Teknolojia ya 5G kutoka Apple
Uwezo wa mashine inayotumika kufanya matengenezo ya iPhone
iPhone calibration – baada ya simu kufanyiwa marekebisho ina uwezo wa kuhakiki mguso wa 3D pamoja na multi-touch ndani ya dakika kumi na tano jambo linakubaliana na viwango vya Apple.
Kitendo cha Apple kurushu kampuni nyingine (Third party) ni jambo jema litakalopunguza kama si kuondoa kabisa ile adha ya kwenda kwenye duka la Apple ili simu yako iweze kurekebishwa na ni matumaini ya wengi kuwa vibali vitatolewa kwa wingi duniani kote.
Chanzo: Engadget, Softpedia