Vita katika kuifanya simu janja iweze kufanya kazi vyema ndio kitu ambacho kinafanya makampuni mbalimbali kutoa simu ambazo zina RAM kubwa na hivyo kufanya kuvutia watu wengi.
Katika hali iilyowashangaza wengi Huawei kwa mara ia kwanza kabisa kupitia bidhaa ambayo inauzwa chini ya yake nikimaanisha Honor imetoa simu ambayo ina RAM yenye ukubwa wa GB 8; hakuna simu yoyote ya Huawei au Honor yenye RAM ya ukubwa huo, Honor 10 GT ndio ya kwanza.
Sifa za Honor 10 GT.
Ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja tu kupita tangu Honor 10 itoke Huawei wameleta toleo jingine ambalo lina tofauti ndogo na mtangulizi wake na hivyo ukizingalia kwa haraka haraka simu zote mbili inakuwa ni vigumu kubaini tofauti zao.
Kioo/Muonekano. Simu hii ina ukubwa wa kioo chenye inchi 5.8|uwiano wa 19:9 (2280 x 1080 LCD) na kimuonekano ni kama ule wa simu janja za karibuni; kuwa na sifa umbo la herufi V (notch) kwenye kioo na ile teknolojia ya usalama kwa kutumia kidole imewekwa kwenye kitufe cha nyumbani.
Prosesa. Honor wameendelea na mtindo wake uleule kama ilivyo kwenye Honor 10 kwa kutumia aina ileile ya prosesa yaani Kirin 970. Betri yake ina uwezo wa 3400mAh.
Kamera. Kwenye kamera ya mbele ina MP 24 mahususi kabisa kwa ajili ya selfie na kwa upande wa nyuma kuna kamera mbili; moja ikiwa na MP 16 na nyingine ina MP 24.
Memori ya ndani/Bei. Honor 10 GT ina diski uhifadhi wenye ukubwa wa GB 128; memori ambayo inaweza kubeba vitu lukuki na wala usihisi kama simu imezidiwa uwezo kutokana na kuwa na vitu vingi. Ingawa bei yake haijawekwa wazi lakini inategemewa kugharimu zaidi ya $390|Tsh. 897,000
Mengineyo kuhusu Honor 10 GT.
Inatumia mfumo endeshi wa Android 8.1, USB Type-C, uwazi mdogo (3.5mm) kwa ajili ya spika za masikioni na inatumia kadi mbili za simu pamoja na kushika mawasiliano ya mpaka 4G LTE.