Simu janja nyingi tuu zimeendelea kuzinduliwa bila kuwasahau Samsung ambao kwa mara nyingine tena wametambulisha Galaxy F22 tayari kwa ajili ya wateja duniani kote.
Mara nyingi tuu TeknoKona tumekuwa tukiandika makla mbalimbali zinazohusu uchambuzi wa simu janja zinazotengenzwa na kampuni kubwa duniani. Samsung ni moja ya kampuni hizo ambazo zimekuwa mstari wa mbele kuleta rununu mbele ya macho ya watu tayari kwa kunufaika kwa kile ambacho wamekitengeneza.
Leo hii katika pita[ita zangu nimekutana na simu janja, Samsung Galaxy F22 ambayo imejaa mengi ya kuvutia katika ulimwengu huu wa teknolojia unapopanuka kila sekunde. Kwa haraka haraka nikaona si vibaya nikawashirikisha wasomaji wetu undani wa rununu husika kama ifuatavyo:-
Ubora wa kioo|Kipuri mama
Kwa kuanza kabisa simu janja hii ambayo naielezea hapa kioo chake kina urefu wa inchi 6.4, ung’avu wa hali ya juu sana-Super AMOLED sawa na 90Hz. Katika hali ya kuifanya simu hii ifanye kazi vizuri kuendana na ambacho kinatakiwa sokoni kipuri mama ni Helio G80.
Uwezo wa betri|Kamera
Macho ya watu wengi duani katika miaka ya karibuni ni uwezo wa betri kwenye simu husika kitu ambacho kinaweza kuwa chachu ya rununu kuuzika sana/kuvutia wateja au la! Simu hii ina 6000mAh (saa 29 kwa matumizi ya intaneti tu, saa 35 za kuangalia picha mnato pekee, saa 133 za kusikiliza muziki na saa 45 iwapo itatumia kwa ajili ya kuongea tu). Upande wa kamera zipo nne (4) (MP 8, 2, 48 na 2) na moja mbele yenye MP 13.
Diski uhifadhi|Mengineyo
Kipengele cha memori kwenye simu janja huwa kina mvuto wa kipekee hasa katika ulimwengu huu wa kisasa zaidi. Simu hii inapatikana katika toleo mbili tofauti kwa maana ya kwamba RAM ni GB 4 au 6, diski uhifadhi-GB 64/128 lakini inawezekana pia kuweka memori ya ziada.
Julai 13 ndio simu hii itaingia sokoni ambapo bei yake ni $170 (4/GB 64)|zaidi ya Tsh. 391,000 au $195 (6/128)|zaidi ya Tsh. 448,500 bei ya India.
Vyanzo: GSMArena, Samsung
No Comment! Be the first one.