CEO wa OnePlus bwana Pete Lau alisema kuwa OnePlus na Oppo kwa pamoja makumpuni hayo mawili yanakua pamoja bega kwa bega ili kuhakikisha kwamba yanaleta bidhaa nzuri sokoni.
Sasa ikishakua hivi unaweza ukajiuliza nani ni nani hapa? maana makampuni yote mawili yanafanya kazi na kuzalisha bidhaa zinazofanana karibia asilimia mia.
Hapa kwa kwamba OnePlus inakua ni brand ya Oppo (na kuwa chini ya Oppo). Ifahamike kuwa Oppo nayo ipo chini ya kampuni ambayo inajulikana kama BBK Electronics.
Kama bado hujaelewa ni kwamba iko hivi BBK Electronics > Oppo > OnePlus. Kingine amnacho kimeelezwa ni kwamba bado kampuni hizo mbili zinaweza kufanya mambo yanayojitegemea.
Katika muunganiko huo, Bwana Lau ambaye ndio/alikua mkuu wa OnePlus moja kwa moja ndiye atakae kuwa mkuu kabisa wa kitengo cha bidhaa (uzalishaji).
Ni wazi kuwa brand hizo zitafanya kazi kwa kujitegemea kila moja lakini vile vile kumbuka kampuni mama ambayo ni BBK Electronics bado inamiliki brand kubwa kama vile Vivo na RealMe.
Naweza kusema kuwa brand za OnePlus na Oppo kulingana na muunganiko huu ni kwamba zitzweza kupata malighafi kwa haraka zaidi ili kuhakikisha kawa zinakuja na bidhaa nzuri zaidi katika soko.
Bado kuna tetesi kuwa bado uhusiano huu haujawekwa hadharani kwa baadhi ya vitu. Bado haipo wazi sana kwa makampuni yote mawili kwamba yatakuwa yanajihusisha na nini kwa mwenzake.
No Comment! Be the first one.