Huduma ya kuweka namna za siri kwenye kadi zetu za simu limekuwepo kwa miongo mingi tuu halikadhalika wengi tuu waliachana na matumizi kadi fulani ya simu kutokana na kupoteza namba za PUK!
Mimi ni mmojawapo wa watu ambao nilikuwa napata changamoto sana tuu hasa pale ambapo nilikuwa nasahau namba za PUK ama kwa namna moja au nyingine nimepoteza ile kadi ya simu ambayo inakuwa na namba za siri (PIN), namba za kuweza kufungua kadi ya simu mara mtu anapokosea namba ya siri.
Miaka mingi baadae mambo yamebadilika, teknolojia imekuwa kiasi kwamba mtu anaweza kupata namba za PUK kwa kuwasiliana na huduma kwa wateja kisha kufuata maelekezo husika kuweza kuanza hatua ya kufungua kadi yake ya simu. Hicho ni kitu kizuri lakini kilichonivutia zaidi ni njia rahisi ya kupata namba za PUK bila kupiga namba ya huduma kwa wateja.
Tigo Tanzania wameongeza kipengele kipya kwenye menyu ya *147*00# kisha kuchagua “Language/Huduma kwa wateja”>>Pata PUK>>Utaweka tarakimu kumi za namba yako ya simu>>Kuweka namba zako za NIDA baada ya hapo utapokea ujumbe mfupi wa maandishi ukiwa namba za PUK (Personal Unblocking Key) zinazohusu namba ya simu husika.
0623366266
Laini yangu 0755350649 imejifinga insdai puk nafanyaje?
Nafikri Voda wana huduma ya mteja kujihudumia mwenyewe kuhusu namna ya kupata PUK lakini ambacho nina uhakika nacho ni lazima utaombwa namba za NIDA ulizotumia kusajili laini husika. Hivyo, tafuta mtu mwingine mwenye laini ya Voda akusaidie kufanikisha huo mchakato.