Makampuni mengi ambayo yanatengeneza simu janja yameshajitosa kwenye ulingo wa rununu ambazo zinakunjika halikadhalika kukunjuka na ujio wake katika mtindo mwingine, teknolojia bora zaidi kuliko ile ya awali imezifanya kupokelewa vizuri sokoni.
Google wamekuwa hawapo mbali kuleta simu janja yao ya kwanza ambayo ipo katika mtindo wa kukunja na kukunjua na zimekuwepo taarifa mbalimbali kuhusu jina la rununu hiyo ambapo awali ilifahamika kuwa kifaa hicho cha mawasiliano kitaitwa Pixel Fold lakini sio hivyo na badala yake inaitwa Pixel Notepad.
Kwa mujibu wa jina hilo tu utagundua kuwa simu janja hiyo inatoka kwenye familia ya rununu zinazotengenezwa na Google ziitwazo Google Pixel ambapo hivi sasa zimefikia toleo la sita. Kwenye Pixel Notepad kuna mambo kadha wa kadha ambayo inafanana na ndunguze mfano simu hii ilitakiwa kuwa na kamera ya MP 50 (kama ilipo kwenye Piexel 6) lakini ikawekwa pembeni kutokana na wembamba wake (thickness). Badala yake simu hii imewekwa kamera kuu yenye MP 12.2 kama ilivyo kwenye Pixel 2 mpaka ya 5.
Inaaminika kuwa simu hii pia itakuwa na mera yenye MP 12 halikadhalika nyingine mbili za MP 8 kila moja kwa ajili ya kamera ya mbele moja simu ikiwa imefunguliwa kwa upana na nyingine ikwa katika muonekano wa inapokuwa imekunjwa. Mbali na hilo simu janja husika inaelezwa kufanana kwa karibu zaidi na Oppo Find N kuliko Samsung Galaxy Z Fold3 na kwa mantiki hiyo Pixel Notepad itakuwa ni fupi zaidi na pana.
Ujio wa Pixel Notepad unatazamiwa kuwa mwisho wa mwaka 2022 na bei yake inatajwa kukaribia $1,400|zaidi ya shilingi za kitanzania 3,220,000. Simu hii inaizidi $400 Galaxy Z Fold3. Je, una neno lolote kuhusiana na simu hii? Tuandikie.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.