Ulimwengu wa sasa unaenda kasi kwa teknolojia ya 5G halikadhalika makampuni mbalimbali yamekuwa yakitoa simu janja ambazo zinakubali hapo tulipofikia hadi sasa na moja ya rununu hizo ni simu janja Samsung Galaxy A22 5G.
Mwezi Juni wakati simu janja Samsung Galaxy A22 4G inazinduliwa toleo la 5G lilitambulishwa pia ambapo rununu hizi zinafanana kwa mengi tuu mbali na muonekano wake lakini hata sifa zake za ndani zinazidiana kwa kiasi fulani ila kiujumla inaweza kuwa ngumu kidogo kuzitofautisha kwa macho. Hizi ndio sifa za simu janja Samsung Galaxy A22 5G:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.6
- Ubora: TFT (1080*2400px, 90Hz); ung’avu wa hali ya juu sana+ kamera ya mbele imeingia kwa ndani kidogo mithili ya bonde la ufa
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+sehemu ya kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4/6/8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 48, 5 na 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1152px
- Kamera ya Mbele: MP 8+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W
Kipuri mama :
- MediaTek Dimensity 700 5G
Uzito :
- Gramu 203
Programu Endeshi
- One UI 3.1, Android 11
Rangi :
- Nyeupe, Kahawia, Udhurungi
Simu hii inagharimu $230|zaidi ya Tsh. 529,000 (4/64), $255|zaidi ya Tsh. 586,500 (6/128) na $265|zaidi ya Tsh. 609,500 (8/128) kwa bei za ughaibuni na tayari ipo sokoni. Kumbuka kufuatilia TeknoKona ili uweze kuhabarika halikadhalika kuelimika kuhusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.