Samsung imeshazindua simu janja za uwezo wa kati kadha wa kadha lakini haijafikia mwisho kwani karibu miezi miezi miwili iliyopita walizindua Galaxy A22 4G.
Makampuni mengi (kama si yote) yanayofanya biashara ya simu janja yamekuwa yakijitahidi kutoa rununu ambazo zinalenga watu wenye vipato tofauti halikadhalika wale ambao hawapendi matumizi makubwa kwenye simu janja hizi rununu zenye uwezo wa kawaida wanazipenda pia.
Samsung Galaxy A22 4G ni simu janja ambayo inaangukia kwenye kundi la rununu ambazo uwezo wake si wa juu wala chini bali katikati kutokana na kile ambacho kimewekwa ndani yake. Sifa zake ni hizi:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.4
- Ubora: Super AMOLED (720*1600px, 90Hz); ung’avu wa hali ya juu sana+ kamera ya mbele imeingia kwa ndani kidogo mithili ya bonde la ufa
Memori :
- Diski uhifadhi: 64GB/128GB+sehemu ya kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 4/6
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 48, 8 na mbili zina MP 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 13+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W
Kipuri mama :
- MediaTek Helio G80
Uzito :
- Gramu 186
Programu Endeshi
- One UI 3.1, Android 11
Rangi :
- Nyeupe, Nyeusi, Udhurungi
Bei yake inaazia $205|zaidi ya Tsh. 471,500 (4/64), $249.99|zaidi ya Tsh. 574,977 (4/128) na $251.60|zaidi ya Tsh. 578,680 (6/128) kwa gharama za ughaibuni na tayari ipo sokoni. Kumbuka kufuatilia TeknoKona ili uweze kuhabarika halikadhalika kuelimika kuhusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.