Wakati mwingine si lazima shamrashamra ziwepo kuonyesha/kutangazia umma kitu fulani bali unaweza kutumia njia mbadala na kufanikisha jambo lako na hivyo ndivyo ilivyozinduliwa Samsung Galaxy A11; mambo yalienda kimyakimya.
Kwa wale wapenzi na wafuatiliaji wa simu janja za Samsung wanafahamu fika kuna matoleo tofauti tofauti ya rununu kutoka familia ya Galaxy A (A10, 10s, A20, n.k). Hivi karibuni kampuni hiyo yenye makao makuu yake Japan iliamua kuweka bidhaa hiyo mpya kwenye tovuti yao tu bila kuiandalia uzinduziambapo watu, wanahabari wangeweza kualikwa kushuhudia tukio hilo.
Simu hiyo ambayo inaelezwa kuwa ya uwezo wa kati ina sifa za kuvutia na pengine kuleta ushawishi hivyo basi kuongeza mapato kwa kampuni husika lakini hata ushindani kwa bidhaa nyinginezo. Samsung Galaxy ina sifa zifuatazo kama zilivyoainishwa kwenye jedwali lifuatalo:-
Kipengele |
Uwezo |
Kioo | Inchi 6.4 LCD (720*1560px) |
Kipuri mama+Kasi yake | Octa-core 1.8 GHz |
Kamera |
Nyuma: Kuna kamera tatu-MP 13, MP 5 na MP 2 + LED flash Mbele: MP 8 ya muundo wa duara dogo |
Diski uhifadhi |
RAM: GB 2 na GB 3 Memori ya ndani: GB 32 + 32GB ya uhifadhi wa ziada |
Mengineyo |
Ulinzi wa kutumia alama ya kidole umewekwa kwa nyuma, betri lina uwezo wa 4000mAh, inatumia kadi mbili (2) za simu, inapatikana kwa rangi Nyeusi, Nyekundu, Nyeupe, Bluu. |
Bado haijajulikana lini itaingia sokoni wala bei yake lakini haitakuwa ya ghali kutokana kuwa kwenye kundi la simu zenye ubora wa katikati.
Vyanzo: GSMArena, Tech Radar