Kwa mujibu wa sheria kwenye nchi nyingi tuu ni lazima kampuni zisajiliwe kwenye soko la hisa ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kununua hisa na kuwa sehemu ya wamiliki wa kampuni husika.
Meta ambayo hapo awali iliitwa Facebook imekuwepo kwenye soko la hisa kwa miaka mingi tuu ambapo thamani yake ilikuwa ikifikia $1 trilioni lakini kwa mwezi Februari 2022 mambo yanaenda vibaya na kufanya mauzo yao ya hisa kushuka kwa 46% kulinganisha na mwaka jana.
Wakati fulani huko nyuma Meta (Facebook) ilikuwa inashika nafasi ya sita kama moja ya makampuni yenye thamani kubwa ulimwenguni lakini sasa hali imebadilika hadi kufikia $565 bilioni na kufanya kushika nafasi ya 11 nyuma ya Tencent Holdings.
Nafasi ya 6 safari hii inashikiliwa na Tesla na thamani yake kwenye soko la hisa imefikia $905.7 bilioni. Nyuma yake ipo Amazon thamani yake ni $1.6 trilioni. Kampuni ya kutengenza magari yanayotumia nishati ya umeme (Bershire Hathaway) ni namba saba-$700.6bn. Nafasi ya nane inashikiliwa na kampuni inayojishughulisha na utengenezaji wa vipuri mama, Nvidia-$613bn.
Kinara ni Apple akiwa na $2.8 trilioni akifuatiwa na Microsoft-$2.2 trn. Nafasi ya tatu ni Aramco-$2trn na anayefuata ni Alphabet-$1.8 trilioni. Je, wewe ni mtu unayemiliki sehemu ya kampuni fualni?
Vyanzo: Bloomberg, The Straits Times
No Comment! Be the first one.