Kila siku teknolojia inakuwa na hii inatokana na mahitaji ya wadau kusababisha wataalamu kufikiria namna gani ya kuweza kutatua jambo fulani kwa wanufaa ya wadau/watumiaji. Kwenye WhatsApp huenda tukawa na uwezo wa kuamua mazungumzo kujifuta baada ya muda fulani kupita.
Utaonekana upo nyuma katika utandawazi iwapo hutumii simu ambayo ina WhatsApp au hata kukosa taarifa fulani kutoka kwa ndugu, jamaa/marafiki kwa sababu tu hutumii programu yenye watumiaji wengi zaidi duniani. Sasa hii ambayo wahusika wanaifanyia majaribio inaweza kuwafurahisha wengi na kuwachukiza wachache 😀 😀 😀 .
Sikii hii: Matoleo mawili ya majaribio (2.80.83 na 2.80.84) kuna kipengele kipya ndani ya mazungumzo ya faragha ambacho kinamuwezesha mhusika kuamua muda gani ujumbe/jumbe alizotuma zijifute mara tu saa, siku, n.k kutimia.
Sisi watumiaji wa WhatsApp tuna mambo mengi na si ajabu tukasahau kuwa tumebadilisha mpangilio kidogo sasa basi mara baada ya kuruhusu mabadiliko ujumbe utakotuma utaambatana na taarifa ya kukukumbusha baada ya muda fulani mazungumzo hayo yatafutika.
Niishie tuu kwa kusema kuwa kipengele hicho bado kipo katika hatua za majaribio kwa whanaotumia matoleo hayo mawili niliyoyaanisha huko juu. Pengine maboresho hayo yakashangiliwa ama kuleta ugomvi kwa namna moja au nyingine 😛 😛 😛 .
Vyanzo: GSMArena, WABetaInfo