Ni wazi TikTok ni moja kati ya mtandao ya kijamii ambao inapata ukuaji mkubwa sana kwa kipindi cha muda mfupi
Licha ya mafanikio hayo bado mtandao wa TikTok unajulikana kama njia kubwa sana inayotumika na watu katika kugundua vipaji
Vipaji hivyo ni kadha wa kadha ikiwemo na ugunduzi wa vipaji vya mziki. Kupitia mtandao huo wa TikTok vipaji vingi sana vimegunduliwa
Mitandao ya kijamii huwa na kawaida kuwa na nguvu kubwa sana katika ugunduzi wa vipaji. Unakumbuka Justin Bieber alivyogunduliwa na meneja wake kupitia mtandao wa kijamii wa Youtube? Fikiri ukubwa wa Justin Bieber sasa?
Turudi TikTok, kampuni ambayo inamiliki mtandao huu (ByteDance) ni kampuni ambayo ina biashara nyingi sana ambazo zinahusisha mtandao.
Ni wazi kuwa masoko mengi ya usambazaji wa muziki yanapata mapato mazuri tuu ukilinganisha na miaka ya zamani, kampuni nalo limeona lisiwe nyuma katika soko hili.
Kwa sasa fununu zinasema kuwa kampuni hiyo mpya ya masuala ya mziki itakwenda kwa jina la TikTok Music na hapa itawawezesha watu kununua, ku’share’ kucheza na kushusha (download) muziki.
Ndio ni kama masoko mengine ya muziki ambayo tumeyazoea kama vile Apple Music na Spotify sio? Kwa hiyo tutegemee mambo yale yale kama vile kuandaa nyimbo-mtiririko pendwa (play List), uwezo wa ku comment pengine na mambo mengine Zaidi
Ningependa kusika kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je utaweza kuachana na huduma zingine za muziki na kuhamia katika huduma hii mpya?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!…
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.