Huduma ya kulipia kupitia mtandao wa Twitter inayojulikana kama Twitter Blue ina mambo mengi na ya kuvutia ukilinganisha na Twitter ya kawaida.
Kuna wengi wanaona kamaa Twitter ya kawaida ni mtandao wa kijamii ambao unawatosha kwa kila kitu lakini kuna wengine ambao wanaona ni bora kwenda katika mtandao wa Twitter Blue ambao ni wakulipia.
Bei ya malipo kwa sasa imepanda kutokea dola 2.99 za kimarekani kwa mwezi mpaka kufikia dola 4.99 za kimarekani kwa mwezi, hili likiwa ni ongezeko la dola 2 nzima.
Kwa ongezeko hili ni kubwa sana lakini kwa wale wapenzi wa dhati wa mtandao huo ni kwamba bado watakua una uwezo wa kumudu kulipia huduma ya mtandao huu kwa mwezi.
Lakini vile vile sio lazima kutumia mtandao huu, utaweza kurudi katika mtandao wa Twitter ule wa kawaida na kuendelea kufurahia huduma za Twitter.
Kwa sasa Twitter Blue inasema kuwa ongezeko hilo la bei litahusisha moja kwa moja kwa wateja wapya. Kwa wateja wa muda mrefu (ambao bado wanaumia huduma hii) kutakua na afadhali kwao—kidogo.
Ni kwamba kwa wale wa zamani ni bado watalipia kiasi kile kile mpaka mwezi oktoba na kasha baada ya hapo wanaweza wakaamua wenyewe kusitisha huduma hiyo au kuanza kulipia kabla ya wengine.
Kwa namba nyingine ni kwamba wateja hawa wapewe dirisha la mwezi mmoja ili kuamua kuwa wataendelea na huduma hiyo huku bei ikiwa imeongezeka au lah.
Ningependa kusikia kutoka kwako, je kama ingekua ni wewe unatumia mtandao huu na wakaongeza dola 2 nzima, je ungekua na uwezo wa kuendelea kutumia mtandao huo au ungeachana na huduma hiyo.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.