Katika makampuni ya kiteknolojia, Apple ilikua imewaacha wenzake mbali sana katika thamani ya soko. Ni wazi wakati wengine wanajikongoja Microsoft ilionekana kufukuzia.
Nilishaandika makala kadhaa kuhusiana na thamani za makampuni haya ya kiteknolojia unaweza kusoma zaidi >> Hapa << >> Facebook << >>Microsoft <<
Lakini pia inavyosemekana ni kutokana na uhafifu wa mauzo katika bidhaa za Apple, ni wazi kwamba tangia iPhone 13 itoke haikupata wateja wengi pengine kama Apple ilivyokua inatarajia
Ukaichana na hayo kwa upande wa Microsoft, ni kwamba imejipatia mauzo mengi katika bidhaa zake za windows, ujazo uhifadhi wa mtandaoni n.k.
Unaweza kuona thamani ya makampuni yote ya kiteknolojia >> Hapa <<
Maono yangu ni kwamba kwa sasa Microsoft itatamba kwa kukaa hapo kileleni lakini haitakaa sana, naamini Apple watarudi katika nafasi yake kwani hawajapishana sana
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Hii Umeipokeaje? Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.