Naam, Microsoft na wenyewe wafikia thamani ya dola trilioni mbili za kimarekani, hii inawafanya wawe wa pili nyuma ya Apple ambao mpaka sasa wapo kidedea.
Vyanzo mbalimbali kama vile CNN na Techtimes viwemeka moja ya sababu ya kampuni hiyo kuongezeka thamani ni kuhuishwa na gonjwa zima la CORONA.
Ijulikane kwamba kwa kipindi cha gonjwa hili wengi walikua wanajifungia ndani (lock down) na hiyo uhitaji wa vitu kama vile kompyuta, simu na magemu viliongezeka sana.
Hali iliyopelekea kampuni ya Microsoft kuweza kuuza bidhaa zake nyingi katika jamii na kupelekea kufanya vizuri katika soko. Ufanyaji wake vizuri katika soko ulifanya mpaka kupanda kwa hisa zake.
Kampuni imefikia thamani ya dola trilioni mbili katika soko ikiwa ni baada ya miaka miwili baada ya kufikisha thamani ya dola trilioni moja.
Amazon na Google nao wanaonekana wakiwa katika harakati za kupambana kwamba wanafikia thamani hiyo ya dola trilioni mbili maana kwa sasa wapo kwenye dola trilioni moja za kimarekani kama thamani ya soko.
No Comment! Be the first one.